Mmmh mmmh
Mama ananiambia Nasibu
Mimi ni mtu mzima na we ndo nakutegemea
Yanayotokea jaribu kupiga kimya
Usidiriki hata kuongea

Mara nasikia vya aibu
Konda Gwajima eti ugomvi umekolea
Kuchunguza karibu
Ni binti mmoja kwa mitandao anachochea

Najariibu kunyamaza, ila moyo utaki
Unaniambia eti Simba japo nguruma uisemee haki
Oooh najaribu kunyamaza hata Laizer hataki ooh
Anasema walau nena kidogo

Na mashabiki Dangote
Wananiambia mbona husemi chochote
Aah si uko nao siku zote, ama ulezi unafanya uogope
Aah na media pande zote wanalalama kiongozi Atoke
Nchi inaingia matope
Niende wapi na mi mtoto wa wote

Acha nikae kimya (nisiongee)
(Kimya) ooh ninyamaze mimi
Nikae kimya, nisiseme (kimya)

Mama kanambia (wacha nikae kimya)
Oooh nifunge mdomo (kimya)
Mie bado mdogo sana (kimya), nisiseme (kimya)

Mmmh ni mengi majaribu najitahidi epuka yasijeni-cost
Japo mengine swadakta mengine hayana maana
Rafiki kipenzi wakaribu ata nyimbo yake sikueza ipost
Ila alivokamatwa iliniumiza sana

Mitandao kila kona
Uongo na ukweli unashonwa
Kila nyumba inanongona
Aaah Ooh Tanzania

Mara kimbembe Dodoma
Bunge wapinzani wameg’oma
Juzi akapotea na Roma
Ooooooh Tanzania ooooh

Najariiibu kunyamaza
Makame hataki oooh eh
Ananiambia walau nena kidogo

Nyumbani nafungua geti
Niende kwa mangi nunua spaghetti eeh
Napewa za chini ya kapeti
Kuna redio imevamiwa eti

Eeh napita kwenye magazeti
Nakuta rundo la watu wameketi eeh
Badala ya kutafuta senti
Wanabishana tu mambo ya vyeti

Wacha nikae kimya (oh nisiongee)
(Kimya) ninyamaze kabisa (nikae kimya)
Ulimi koma (kimya)
Usijekuniponza (wacha nikae kimya)

Nifunge bakuli langu (kimya)
Nikojoe nikalale (nikae kimya)
Me bado mudogo sana (kimya)
Mama kanambia

Ooooh najiuliza (wapi)
Najiuliiza (wapi)
Tunakwenda wapi (wapi)
Kila siku maneno (wapi)
Ah tuacheni jamani (wapi)

Me na we ni taifa moja (wapi)
Kambarage baba mmoja (wapi)
Sa tofauti za nini tushikamane (wapi)
Tukaijenge Tanzania

Share: Acha Nikae Kimya Lyrics by Diamond Platnumz

📣 Do you find Musiclyfer useful? Follow us on Facebook(@musiclyfer) and stay updated.